Yohana 16:1-4
1
“Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
2
Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
3
Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
4
Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
Settings