Yohana 12:37-40
37
Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
38
Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
39
Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
40
“Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
Settings