Skip to content
Yohana 11:17-37

Yohana 11:17-37

17
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
19
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
21
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
22
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
26
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?”
27
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
30
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
32
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
33
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
35
Yesu akalia machozi.
36
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options