Ayubu 9:14-20
14
“Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye?
15
Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie.
16
Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.
17
Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.
18
Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.
19
Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?
20
Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.
Settings