Ayubu 4:14-17
14
hofu na kutetemeka kulinishika na kufanya mifupa yangu yote itetemeke.
15
Kuna roho aliyepita mbele ya uso wangu, nazo nywele za mwili wangu zikasimama.
16
Yule roho akasimama, lakini sikuweza kutambua kilikuwa kitu gani. Umbo fulani lilisimama mbele ya macho yangu, kukawa na ukimya kisha nikasikia sauti:
17
‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu? Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?
Settings