Ayubu 39:1-3
1
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
2
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.