Ayubu 38:25-27
25
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?