Skip to content
Ayubu 36:26-32

Ayubu 36:26-32

26
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options