Skip to content
Ayubu 34:31-37

Ayubu 34:31-37

31
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options