Ayubu 34:21-27
21
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Settings