Ayubu 28:1-4
1
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Settings