Ayubu 13:7-11
7
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
Settings