Skip to content
Yeremia 6:1

Yeremia 6:1

Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
“Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
2
Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
3
Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
4
“Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options