Skip to content
Yakobo 4:6-10

Yakobo 4:6-10

6
Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema: “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
7
Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia.
8
Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili.
9
Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni.
10
Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options