Skip to content
Isaya 9:8-12

Isaya 9:8-12

8
Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
9
Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
10
“Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
11
Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
12
Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options