Skip to content
Isaya 7:10-16

Isaya 7:10-16

10
Bwana akasema na Ahazi tena,
11
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.”
12
Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
13
Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
14
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
15
Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
16
Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options