1
Jangwa na nchi kame vitafurahi; nyika itashangilia na kuchanua maua. Kama waridi,
2
litachanua maua, litashangilia sana na kupaza sauti kwa furaha. Litapewa utukufu wa Lebanoni, fahari ya Karmeli na Sharoni; wataona utukufu wa Bwana, fahari ya Mungu wetu.