Skip to content
Isaya 3:12-15

Isaya 3:12-15

12
Vijana wanawatesa watu wangu, wanawake wanawatawala. Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha, wanawapoteza njia.
13
Bwana anachukua nafasi yake mahakamani, anasimama kuhukumu watu.
14
Bwana anaingia katika hukumu dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake: “Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu, mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.
15
Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu na kuzisaga nyuso za maskini?” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options