Rukia maudhui
Isaya 3:1-7

Kuondolewa kwa Msaada na Uongozi

Isaya 3:1-7
1
Tazama sasa, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda upatikanaji wa mahitaji na misaada, upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
2
shujaa na mtu wa vita, mwamuzi na nabii, mwaguzi na mzee,
3
jemadari wa kikosi cha watu hamsini na mtu mwenye cheo, mshauri, fundi stadi na mlozi mjanja.
4
Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao, watoto ndio watakaowatawala.
5
Watu wataoneana wao kwa wao: mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake. Kijana atainuka dhidi ya mzee, mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
6
Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake katika nyumba ya baba yake na kusema, “Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu, tawala lundo hili la magofu!”
7
Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema, “Sina uponyaji. Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu, msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options