Rukia maudhui
Isaya 10:20-23

Mabaki Yatarudi

Isaya 10:20-23
20
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options