Mwanzo 32:22-24
22
Usiku ule Yakobo akaamka akawachukua wake zake wawili, watumishi wake wawili wa kike na wanawe kumi na mmoja na akavuka kivuko cha Yaboki.
23
Baada ya kuwavusha ngʼambo ya kijito, alivusha pia mali zake zote.
24
Kwa hiyo Yakobo akaachwa peke yake na mtu mmoja akashikana naye mweleka mpaka mapambazuko.
Settings