Lumaktaw sa nilalaman
Mwanzo 31:45-49

Mwanzo 31:45-49

45
Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo.
46
Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo.
47
Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi.
48
Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi.
49
Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options