Skip to content
Mwanzo 27:9-17

Mwanzo 27:9-17

9
Nenda sasa katika kundi ukaniletee wana-mbuzi wawili wazuri, ili niandalie chakula kitamu kwa ajili ya baba yako, kama vile anavyopenda.
10
Kisha umpelekee baba yako ale, ili apate kukubariki kabla hajafa.”
11
Yakobo akamwambia Rebeka mama yake, “Lakini ndugu yangu Esau ana nywele mwilini, mimi nina ngozi nyororo.
12
Itakuwaje kama baba yangu akinigusa? Itaonekana kwake kama niliyemfanyia ujanja na kuleta laana juu yangu badala ya baraka.”
13
Mama yake akamwambia, “Mwanangu, laana na iwe juu yangu. Fanya tu ninalokuambia, nenda ukaniletee hao wana-mbuzi.”
14
Kwa hiyo alikwenda akawaleta, akampa mama yake, akaandaa chakula kitamu, kama vile alivyopenda baba yake.
15
Kisha Rebeka akachukua nguo nzuri za Esau mwanawe wa kwanza, alizokuwa nazo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo.
16
Pia akamfunika mikononi na sehemu laini ya shingo kwa ngozi za mbuzi.
17
Hatimaye akampa Yakobo hicho chakula kitamu pamoja na mkate aliouoka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options