Wagalatia 5:14
Inaonyesha mstari 14 pamoja na muktadha unaouzunguka.
11
Lakini ndugu zangu, kama mimi bado ninahubiri kuhusu kutahiriwa, kwa nini bado ninateswa? Katika hiyo hali basi, kwazo la msalaba limeondolewa.
12
Laiti hao wanaowavuruga wangejihasi wao wenyewe!
13
Ndugu zangu, ninyi mliitwa ili mwe huru, hivyo msitumie uhuru wenu kama fursa ya kufuata tamaa za mwili, bali tumikianeni ninyi kwa ninyi kwa upendo.
14
Kwa maana sheria yote hukamilika katika amri moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.”
15
Kama mkiumana na kutafunana, angalieni, msije mkaangamizana.
16
Kwa hiyo nasema, enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17
Kwa maana mwili hutamani yale yaliyo kinyume na Roho, naye Roho hutamani yale yaliyo kinyume na mwili. Roho na mwili hupingana na kwa sababu hiyo hamwezi kufanya mnayotaka.
Settings