Skip to content
Wagalatia 4:12-16

Wagalatia 4:12-16

12
Ndugu zangu, nawasihi mwe kama mimi, kwa sababu mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea jambo lolote baya.
13
Ninyi mwajua kwamba ni kwa ajili ya udhaifu wangu niliwahubiria Injili.
14
Ingawa hali yangu iliwatia majaribuni, hamkunidharau wala kunidhihaki, bali mlinikaribisha kama malaika wa Mungu, kama vile Kristo Yesu.
15
Ile hali ya furaha mliyokuwa nayo imekwenda wapi? Naweza kushuhudia kwamba, kama ingewezekana mngengʼoa macho yenu na kunipa mimi.
16
Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa kuwaambia kweli?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options