Wagalatia 3:6-9
6
Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
7
Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
8
Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
9
Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
Settings