Wagalatia 3:19-20
19
Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20
Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.