Skip to content
Ezekieli 28:1-5

Ezekieli 28:1-5

1
Neno la Bwana likanijia kusema:
2
“Mwanadamu, mwambie mfalme wa Tiro, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “ ‘Kwa sababu moyo wako umejivuna na umesema, “Mimi ni mungu; nami ninaketi katika kiti cha enzi cha mungu katika moyo wa bahari.” Lakini wewe ni mwanadamu, wala si mungu, ingawa unafikiri kuwa una hekima kama mungu.
3
Je, wewe una hekima kuliko Danieli? Je, hakuna siri iliyofichika kwako?
4
Kwa hekima yako na ufahamu wako, umejipatia utajiri, nawe umejikusanyia dhahabu na fedha katika hazina zako.
5
Kwa werevu wako mwingi katika biashara, umeongeza utajiri wako na kwa sababu ya utajiri wako moyo wako umekuwa na kiburi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options