Rukia maudhui
Kutoka 9:1-7

Pigo la Tano: Tauni Juu ya Mifugo

Kutoka 9:1-7
1
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
2
Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
3
mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
4
Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’ ”
5
Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
6
Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
7
Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options