Kutoka 21:12-17
12
“Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
13
Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
14
Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
15
“Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
16
“Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
17
“Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Settings