Rukia maudhui
Waefeso 3:14-19

Sala ya Paulo kwa Ajili ya Kuimarishwa kwa Ndani

Waefeso 3:14-19
14
Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
15
ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
16
Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
17
ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
18
mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
19
na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options