Mhubiri 3:1-10
1
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
2
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
3
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
4
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
5
wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
6
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
7
wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
8
wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
9
Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?
10
Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.
Settings