Skip to content
Kumbukumbu 32:26-33

Kumbukumbu 32:26-33

26
Nilisema ningewatawanya na kufuta kumbukumbu lao katika mwanadamu.
27
Lakini nilihofia dhihaka za adui, adui asije akashindwa kuelewa, na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda; Bwana hakufanya yote haya.’ ”
28
Wao ni taifa lisilo na akili, hakuna busara ndani yao.
29
Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwa aje!
30
Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja, au wawili kufukuza elfu kumi, kama si kwamba Mwamba wao amewauza, kama si kwamba Bwana amewaacha?
31
Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu, sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.
32
Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kutoka kwenye mashamba ya Gomora. Zabibu zake zimejaa sumu, na vishada vyake vimejaa uchungu.
33
Mvinyo wao ni sumu ya nyoka, sumu yenye kufisha ya swila.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options