Skip to content
Kumbukumbu 28:1-6

Kumbukumbu 28:1-6

1
Kama ukimtii Bwana Mungu wako kwa bidii na kufuata amri zake zote ninazokupa leo kwa bidii, Bwana Mungu wako atakuweka juu ya mataifa yote katika dunia.
2
Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukupata, kama ukimtii Bwana Mungu wako:
3
Utabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani.
4
Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ngʼombe, na wana-kondoo wa makundi yako.
5
Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa.
6
Utabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options