Skip to content
Kumbukumbu 27:15-26

Kumbukumbu 27:15-26

15
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options