Rukia maudhui
Kumbukumbu 11:13-17

Agano la Masharti: Mvua na Ukame

Kumbukumbu 11:13-17
13
Hivyo kama mkiyatii maagizo yangu ninayowapa leo kwa uaminifu, yaani kwa kumpenda Bwana Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wako wote na kwa roho yenu yote,
14
ndipo atawanyweshea mvua katika nchi yenu kwa majira yake, mvua ya masika na ya vuli, ili mpate kuvuna nafaka zenu, divai mpya na mafuta.
15
Nitawapa majani kwa ajili ya ngʼombe wenu, nanyi mtakula na kushiba.
16
Jihadharini, la sivyo mtashawishika kugeuka na kuabudu miungu mingine na kuisujudia.
17
Ndipo hasira ya Bwana itawaka dhidi yenu, naye atafunga mbingu ili mvua isinyeshe nayo ardhi haitatoa mazao, nanyi mtaangamia mara katika nchi nzuri ambayo Bwana anawapa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options