Wakolosai 1:12-14
12
mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
13
Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
14
ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.