Matendo 5:12-14
12
Mitume wakafanya ishara nyingi na miujiza miongoni mwa watu. Walioamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Solomoni.
13
Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kuambatana nao ijapokuwa waliheshimiwa sana na watu.
14
Hata hivyo, waliomwamini Bwana wakazidi kuongezeka, wanaume na wanawake.