Matendo 2:1-4
1
Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
2
Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
3
Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
4
Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
Settings