2 Wafalme 23:31-32
31
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
32
Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.