Skip to content
1 Timotheo 5:11-15

1 Timotheo 5:11-15

11
Lakini kwa habari za wajane vijana usiwaweke kwenye orodha hiyo, maana tamaa zao za kimaumbile zikizidi kule kujitoa kwao kwa Kristo, watataka kuolewa tena.
12
Nao kwa njia hiyo watajiletea hukumu kwa kukiuka ahadi yao ya kwanza.
13
Zaidi ya hayo, wajane kama hao huwa na tabia ya uvivu wakizurura nyumba kwa nyumba, wala hawawi wavivu tu, bali pia huwa wasengenyaji, wajiingizao katika mambo yasiyowahusu na kusema mambo yasiyowapasa kusema.
14
Hivyo nawashauri wajane vijana waolewe, wazae watoto na wasimamie nyumba zao, wasije wakampa adui nafasi ya kutushutumu.
15
Kwa maana kwa kweli wajane wengine wamepotoka ili kumfuata Shetani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options