Skip to content
1 Yohana 2:24-28

1 Yohana 2:24-28

24
Hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
25
Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani, uzima wa milele.
26
Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
27
Nanyi, upako mlioupata kutoka kwake unakaa ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
28
Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options