Skip to content
1 Wakorintho 9:1-6

1 Wakorintho 9:1-6

1
Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana?
2
Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni mhuri wa utume wangu katika Bwana.
3
Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu.
4
Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5
Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini, kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana na Kefa?
6
Au ni mimi na Barnaba tu inatubidi kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options