1 Wakorintho 4:18-21
18
Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu.
19
Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao.
20
Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu.
21
Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?
Settings