Skip to content
1 Wakorintho 14:1-5

1 Wakorintho 14:1-5

1
Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
2
Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
3
Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
4
Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
5
Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options