Skip to content
1 Wakorintho 12:3

1 Wakorintho 12:3

Inaonyesha mstari 3 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5
Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
6
Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options