Skip to content
1 Wakorintho 10:5-12

1 Wakorintho 10:5-12

5
Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
6
Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
7
Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
8
Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
9
Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
10
Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
11
Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia.
12
Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.

Jifunze kifungu hiki

Ufafanuzi wa kifungu hiki, si mstari mmoja.

Maandiko mengine yanaposema hivi.

  • Warumi 15:4

    Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.
    kutoka mstari wa 11
  • Warumi 11:20

    Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.
    kutoka mstari wa 12
  • 2 Petro 3:17

    Basi, ninyi wapenzi, kwa kuwa mmekwisha kujua mambo haya, jilindeni msije mkachukuliwa na kosa la watu hao waasi na kuanguka kutoka kwenye uthabiti wenu.
    kutoka mstari wa 12
  • Mithali 16:18

    Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.
    kutoka mstari wa 12
  • Kutoka 32:6

    Kwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha katika sherehe.
    kutoka mstari wa 7
  • Kutoka 32:8

    Wamekuwa wepesi kugeuka na kuacha niliyowaamuru, na wamejitengenezea sanamu ya kuyeyusha yenye umbo la ndama. Wameisujudia na kuitolea dhabihu, nao wamesema, ‘Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli iliyokupandisha kutoka Misri.’ ”
    kutoka mstari wa 7
  • Hesabu 25:1

    Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
    kutoka mstari wa 8
  • Hesabu 25:9

    Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
    kutoka mstari wa 8
  • Mathayo 26:40

    Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
    kutoka mstari wa 12
  • Mathayo 26:41

    Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
    kutoka mstari wa 12
  • 1 Wakorintho 8:2

    Mtu yeyote anayedhani kwamba anajua kitu, bado hajui kama impasavyo kujua.
    kutoka mstari wa 12
  • Hesabu 21:5

    wakamnungʼunikia Mungu na Mose, wakisema, “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili tufe jangwani? Hakuna mkate! Hakuna maji! Nasi tunachukia sana chakula hiki duni!”
    kutoka mstari wa 9
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options