Skip to content
1 Nyakati 23:12-18

1 Nyakati 23:12-18

12
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options