Rukia maudhui

Zaburi93

Bwana Anatawala Milele

1
Bwana anatawala, amejivika utukufu; Bwana amejivika utukufu tena amejivika nguvu. Dunia imewekwa imara, haitaondoshwa.
2
Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani; wewe umekuwako tangu milele.

Uweza wa Mungu Juu ya Mafuriko

3
Bahari zimeinua, Ee Bwana, bahari zimeinua sauti zake; bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.
4
Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu, ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari: Bwana aishiye juu sana ni mkuu.

Uaminifu na Utakatifu

5
Ee Bwana, sheria zako ni imara; utakatifu umepamba nyumba yako pasipo mwisho.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options