- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi33
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mwito wa Kusifu kwa Furaha
1
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Haki na Kweli ya Neno la Mungu
4
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Mungu Muumba Mwenye Enzi
6
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Shauri la Bwana la Milele
10
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Bwana Anawalinda Watu Wake
12
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Tamko la Mwisho la Kumtumaini Mungu na Ombi
20
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note